Kala coming soon
Msanii mwingine anayetarajia kuachia wimbo mpya hivi karibuni na rapperKala Jeremiah, wimbo wake unaitwa Usikate tamaa akiwa amemshirikisha msanii wa R&B wa muda mrefu Nuruwell, msanii ambaye miaka michache iliyopita alipotea kwenye bongo fleva.
Kala ameiambia Bongo5 kuwa bado hana tarehe kamili ya lini wimbo wake utatoka kwasababu bado kuna mambo anayakamilisha, lakini utatoka siku si nyingi.